

BY EMMANUEL WABOMBA, TMG JOURNALIST.
๐ ๐ฎ๐๐ต๐ถ๐ป๐ฑ๐ฎ๐ป๐ผ ๐๐ฎ ๐ ๐ฝ๐ถ๐ฟ๐ฎ ๐๐ฎ ๐ช๐ฎ๐๐ ๐๐ฎ ๐๐ฎ๐ป ๐ช๐ฎ๐ป๐๐ฎ๐บ๐ฎ ๐๐บ๐ฏ๐ผ๐๐ฒ๐น๐ถ – ๐๐น๐ฎ๐ฏ๐ ๐๐ฎ ๐ช๐ฎ๐ป๐ฎ๐๐บ๐ฒ ๐๐ฎ ๐๐ผ๐ธ๐ผ๐น๐ถ ๐ป๐ฎ ๐ฆ๐ต๐๐น๐ฒ ๐๐ฎ ๐จ๐ฝ๐ถ๐น๐ถ ๐๐ฎ ๐ช๐ฎ๐๐ถ๐ฐ๐ต๐ฎ๐ป๐ฎ ๐๐ฎ ๐๐ฒ๐๐ผ๐ด๐ผ๐ป ๐ฌ๐ฎ๐ป๐ด’๐ฎ๐ฟ๐ฎ ๐ธ๐ฎ๐๐ถ๐ธ๐ฎ ๐จ๐๐ต๐ถ๐ป๐ฑ๐ถ ๐๐ฎ ๐จ๐ฏ๐ถ๐ป๐ด๐๐ฎ.
Mashindano ya Dan Wanyama ‘Amboseli Volleyball Tournament’ yamekamilika kwa kishindo huku Klabu ya Wanaume ya Bokoli na Shule ya Upili ya Wasichana ya Kesogon wakitwaa mataji ya ubingwa.Fainali hizo zilifanyika katika uwanja wa Shule ya Upili ya Wavulana ya Bokoli, Kaunti ya Bungoma, na ziliwavutia maelfu ya mashabiki waliojitokeza kushuhudia ushindani wa hali ya juu.
Katika kitengo cha wanaume, Bokoli walidhihirisha umahiri wao kwa kuwashinda Kakamega Kings kwa seti 3-1. Seti ya kwanza ilishuhudia Bokoli wakishinda kwa alama 25-20, kabla ya Kakamega Kings kurejea kwa ushindi wa 21-25 katika seti ya pili. Hata hivyo, Bokoli walionyesha uthabiti na kushinda seti ya tatu na ya nne kwa alama 25-18 na 25-16 mtawalia, na hivyo kutawazwa mabingwa.Kwa upande wa wanawake, Shule ya Upili ya Kesogon kutoka West Pokot waliandika historia kwa kuwashinda Bishop Sulumeti kwa seti 3-2 katika mechi iliyosheheni msisimko na kasi ya hali ya juu.Safari ya mafanikio ya timu hizi haikuwa rahisi.

Bokoli walifuzu fainali kwa ushindi wa seti 3-0 dhidi ya Bungoma Mseto, huku Kakamega Kings wakipata tiketi ya fainali baada ya kuwashinda Merewet ya Uasin Gishu kwa seti 3-0. Kwa upande wa wanawake, Kesogon walifanikiwa kuwashinda Lugulu Girls kwa seti 3-1, hali sawa na Bishop Sulumeti walipowafunga Kosirai kutoka Nandi.Mashindano haya, ambayo yalihusisha shule za sekondari, vyuo, na hata sekondari ya awali, yameibua vipaji na kuonyesha ukuaji wa michezo nchini. Mheshimiwa Dan Wanyama, mfadhili wa mashindano haya, aliwahimiza wachezaji kudumisha nidhamu kama msingi wa kukuza vipaji vyao.Pia alibainisha kuwa serikali imejizatiti kuboresha viwango