

Brigid Sikuku.
Viongozi wa chama cha Ford Kenya katika eneo bunge la Kabuchai wamekutana kujadili mwelekeo wa kisiasa na maandalizi ya mchujo kuelekea uchaguzi mdogo wa wadi ya Chwele.
Hii ni baada ya mmoja wa waliokuwa wagombea, DCC Eric Wanyonyi, kutangaza kujiondoa kwenye kinyang’anyiro hicho ili kuunga mkono mshikamano ndani ya chamaKatika taarifa yake DCC Erick Wanyonyi alitangaza kwa heshima na uwazi kuwa hatawania tena kiti cha MCA katika wadi ya Chwele, akieleza kuwa uamuzi wake umetokana na nia ya dhati ya kuhakikisha mshikamano ndani ya chama na mafanikio ya Ford Kenya katika uchaguzi huo.
“Nimejiondoa katika uchaguzi wa Chwele Kabuchai ambao utafanyika Septemba 27”
Uamuzi huo umepokelewa kwa mikono miwili na viongozi wa chama hicho, wakiongozwa na mwenyekiti wa Ford Kenya katika eneo la Kabuchai, Mheshimiwa Polycarp Wandabusi, ambaye amempongeza Wanyonyi kwa kile alichokitaja kama uamuzi wa kishujaa unaoweka mbele maslahi ya chama na wananchi.”Ningependa kupongeza uamuzi wa ndugu yetu Erick Wanyonyi,ni mfano wa uongozi wa kweli.”Wandabusi alisisitiza kuwa Ford Kenya itaendesha mchujo wake kwa njia
-
Naibu Rais Atoa Tumaini kwa Vijana wa Trans Nzoia.
Share this postBRIGID SIKUKU. Katika hali ya sasa ambapo ukosefu wa ajira unaendelea kuwa changamoto kubwa kwa vijana
-
Murkomen Breaks Silence: “No Jubaland Invasion, But Kenya Won’t Tolerate Chaos”
Share this postFLORENCE SIMIYU. Interior Cabinet Secretary Kipchumba Murkomen has moved to quell fears of an alleged incursion
-
H.E. Mudavadi Vows Continued Support for Haiti: “Corporal Muthwii’s Sacrifice Will Not Be in Vain”
Share this postROBERT WANYONYI. In a solemn and strategic exchange, Kenya’s Prime Cabinet Secretary and Cabinet Secretary for
huru na ya haki, bila upendeleo, ili kumpata mgombea bora atakayepeperusha bendera ya chama hicho kwa kuzingatia maadili, uadilifu na uwezo wa kuhudumia wananchiKwa upande wake, Mkurugenzi wa uchaguzi wa chama hicho, Bi. Khadija Mustapha, aliwahimiza wanachama kujitokeza kwa wingi na kushiriki mchakato huo kwa amani, nidhamu na kuheshimu maamuzi ya chama ili kudumisha mshikamano.
Bi Khadija aliongeza kuwa maandalizi ya mchujo huo yako katika hatua za mwisho, huku kamati ya uchaguzi ikiwahakikishia wanachama wote kuwa kila kura itahesabiwa na sauti ya mwanachama yeyote haitapotea.Katibu wa Ford Kenya katika eneo hilo, Bw. David Milimo, alibainisha kuwa chama hicho kimejipanga kuendeleza kampeni za Amani Na wazi huku kikijitahidi kushughulikia malalamiko yoyote kwa njia ya haki na haraka.
Viongozi hao kwa pamoja walisisitiza kuwa uchaguzi huo ni fursa ya Ford Kenya kuonyesha umoja na nguvu yake katika siasa za mashinani, hasa kwa kuzingatia kuwa Kabuchai ni mojawapo ya ngome muhimu za chama hicho.Kwa sasa macho yote yako kwa Ford Kenya na mchujo wao unaotarajiwa kuvuta hisia si tu za wafuasi wa chama hicho, bali pia za wadau wote wa kisiasa katika kaunti ya Bungoma. Ni wazi kuwa chama hicho kimeweka msingi imara kuelekea uchaguzi mdogo wa wadi ya Chwele.