
Brigid Sikuku.
Viongozi wa chama cha Ford Kenya katika eneo bunge la Kabuchai wamekutana kujadili mwelekeo wa kisiasa na maandalizi ya mchujo kuelekea uchaguzi mdogo wa wadi ya Chwele.
Hii ni baada ya mmoja wa waliokuwa wagombea, DCC Eric Wanyonyi, kutangaza kujiondoa kwenye kinyang’anyiro hicho ili kuunga mkono mshikamano ndani ya chamaKatika taarifa yake DCC Erick Wanyonyi alitangaza kwa heshima na uwazi kuwa hatawania tena kiti cha MCA katika wadi ya Chwele, akieleza kuwa uamuzi wake umetokana na nia ya dhati ya kuhakikisha mshikamano ndani ya chama na mafanikio ya Ford Kenya katika uchaguzi huo.
“Nimejiondoa katika uchaguzi wa Chwele Kabuchai ambao utafanyika Septemba 27”
Uamuzi huo umepokelewa kwa mikono miwili na viongozi wa chama hicho, wakiongozwa na mwenyekiti wa Ford Kenya katika eneo la Kabuchai, Mheshimiwa Polycarp Wandabusi, ambaye amempongeza Wanyonyi kwa kile alichokitaja kama uamuzi wa kishujaa unaoweka mbele maslahi ya chama na wananchi.”Ningependa kupongeza uamuzi wa ndugu yetu Erick Wanyonyi,ni mfano wa uongozi wa kweli.”Wandabusi alisisitiza kuwa Ford Kenya itaendesha mchujo wake kwa njia
-
Kifo cha Sheila Chebii: Familia Yasubiri Majibu Kutoka Australia

Share this postBY VIONA SIMIYU Maswali mazito yanaendelea kuibuka kufuatia kifo cha Sheila Chebii, Mkenya mwenye umri wa miaka 25 aliyefariki nchini Australia katika mazingira ambayo familia yake inasema hayajafafanuliwa kikamilifu. Sheila alikuwa amehamia nchini humo kwa ajili ya masomo na kutafuta fursa bora za maisha. Kwa familia yake iliyoko Kenya, taarifa za kifo hicho…
-
Education Ministry Sounds Alarm Over Ksh 111B Budget Gap

Share this postBY VIONA SIMIYU The Ministry of Education has raised concern over a looming funding shortfall ahead of the 2026/2027 financial year, warning that a deficit of more than Ksh 111 billion could cripple key programmes across the country.Principal Secretary Julius Bitok said Basic Education requires approximately Ksh 246 billion to run effectively, but…
-
Tension in Nanyuki as Protesters Arrested Over Ebola Quarantine Center

Share this postBY CYNTHIA ELIZABETH The town of Nanyuki has been gripped by tension following protests against the planned construction of an Ebola quarantine facility at the Laikipia Air Base.Demonstrators voiced fears about health risks and the lack of public consultation, insisting the project posed a danger to the community. “We as the community at…
huru na ya haki, bila upendeleo, ili kumpata mgombea bora atakayepeperusha bendera ya chama hicho kwa kuzingatia maadili, uadilifu na uwezo wa kuhudumia wananchiKwa upande wake, Mkurugenzi wa uchaguzi wa chama hicho, Bi. Khadija Mustapha, aliwahimiza wanachama kujitokeza kwa wingi na kushiriki mchakato huo kwa amani, nidhamu na kuheshimu maamuzi ya chama ili kudumisha mshikamano.
Bi Khadija aliongeza kuwa maandalizi ya mchujo huo yako katika hatua za mwisho, huku kamati ya uchaguzi ikiwahakikishia wanachama wote kuwa kila kura itahesabiwa na sauti ya mwanachama yeyote haitapotea.Katibu wa Ford Kenya katika eneo hilo, Bw. David Milimo, alibainisha kuwa chama hicho kimejipanga kuendeleza kampeni za Amani Na wazi huku kikijitahidi kushughulikia malalamiko yoyote kwa njia ya haki na haraka.
Viongozi hao kwa pamoja walisisitiza kuwa uchaguzi huo ni fursa ya Ford Kenya kuonyesha umoja na nguvu yake katika siasa za mashinani, hasa kwa kuzingatia kuwa Kabuchai ni mojawapo ya ngome muhimu za chama hicho.Kwa sasa macho yote yako kwa Ford Kenya na mchujo wao unaotarajiwa kuvuta hisia si tu za wafuasi wa chama hicho, bali pia za wadau wote wa kisiasa katika kaunti ya Bungoma. Ni wazi kuwa chama hicho kimeweka msingi imara kuelekea uchaguzi mdogo wa wadi ya Chwele.