
Brigid Sikuku.
Viongozi wa chama cha Ford Kenya katika eneo bunge la Kabuchai wamekutana kujadili mwelekeo wa kisiasa na maandalizi ya mchujo kuelekea uchaguzi mdogo wa wadi ya Chwele.
Hii ni baada ya mmoja wa waliokuwa wagombea, DCC Eric Wanyonyi, kutangaza kujiondoa kwenye kinyang’anyiro hicho ili kuunga mkono mshikamano ndani ya chamaKatika taarifa yake DCC Erick Wanyonyi alitangaza kwa heshima na uwazi kuwa hatawania tena kiti cha MCA katika wadi ya Chwele, akieleza kuwa uamuzi wake umetokana na nia ya dhati ya kuhakikisha mshikamano ndani ya chama na mafanikio ya Ford Kenya katika uchaguzi huo.
“Nimejiondoa katika uchaguzi wa Chwele Kabuchai ambao utafanyika Septemba 27”
Uamuzi huo umepokelewa kwa mikono miwili na viongozi wa chama hicho, wakiongozwa na mwenyekiti wa Ford Kenya katika eneo la Kabuchai, Mheshimiwa Polycarp Wandabusi, ambaye amempongeza Wanyonyi kwa kile alichokitaja kama uamuzi wa kishujaa unaoweka mbele maslahi ya chama na wananchi.”Ningependa kupongeza uamuzi wa ndugu yetu Erick Wanyonyi,ni mfano wa uongozi wa kweli.”Wandabusi alisisitiza kuwa Ford Kenya itaendesha mchujo wake kwa njia
-
ODM War Erupts: Junet, Wandayi Attack Sifuna at Ruto-Funded Rallies

Share this postBY DAPHINE JUMAH ODM’s internal cracks burst into the open over the weekend as a pro-government faction led a fierce attack on Nairobi Senator Edwin Sifuna during a fundraiser in Nairobi.The drama played out in Kileleshwa, Dagoretti North, at an event meant to empower women and boda boda riders. Instead, it turned into…
-
Veteran Journalist Muliro Telewa Dies at 68, Kenya Mourns a Champion of Press Freedom

Share this postBY ALLAN BRADLEY Renowned journalist Muliro Telewa has died at 68 while undergoing treatment at a hospital in Nakuru, ending a media career that shaped Kenya’s democratic journey.According to his family, Telewa had been battling kidney failure for years. The condition was under control, but his health suddenly worsened leading to his death.Telewa…
-
ODM YAVUA GAMBA: Mgombea wa Urais 2027 Atajwa Kabla ya Krismasi

Share this postBY GELAS SITUMA Chama cha ODM kimesema kitamtangaza rasmi mgombea wa urais atakayekiunga mkono 2027 kabla ya mwezi Desemba mwaka huu.Akizungumza Nyanza wakati wa mkutano wa mashauriano na wafuasi, Mwenyekiti Oburu Odinga alisema uamuzi huo utatokana na maoni ya wanachama kote nchini. “Tunataka mgombea wetu awe mtu aliyechaguliwa na wanachama, sio kuamuliwa ofisini.…
huru na ya haki, bila upendeleo, ili kumpata mgombea bora atakayepeperusha bendera ya chama hicho kwa kuzingatia maadili, uadilifu na uwezo wa kuhudumia wananchiKwa upande wake, Mkurugenzi wa uchaguzi wa chama hicho, Bi. Khadija Mustapha, aliwahimiza wanachama kujitokeza kwa wingi na kushiriki mchakato huo kwa amani, nidhamu na kuheshimu maamuzi ya chama ili kudumisha mshikamano.
Bi Khadija aliongeza kuwa maandalizi ya mchujo huo yako katika hatua za mwisho, huku kamati ya uchaguzi ikiwahakikishia wanachama wote kuwa kila kura itahesabiwa na sauti ya mwanachama yeyote haitapotea.Katibu wa Ford Kenya katika eneo hilo, Bw. David Milimo, alibainisha kuwa chama hicho kimejipanga kuendeleza kampeni za Amani Na wazi huku kikijitahidi kushughulikia malalamiko yoyote kwa njia ya haki na haraka.
Viongozi hao kwa pamoja walisisitiza kuwa uchaguzi huo ni fursa ya Ford Kenya kuonyesha umoja na nguvu yake katika siasa za mashinani, hasa kwa kuzingatia kuwa Kabuchai ni mojawapo ya ngome muhimu za chama hicho.Kwa sasa macho yote yako kwa Ford Kenya na mchujo wao unaotarajiwa kuvuta hisia si tu za wafuasi wa chama hicho, bali pia za wadau wote wa kisiasa katika kaunti ya Bungoma. Ni wazi kuwa chama hicho kimeweka msingi imara kuelekea uchaguzi mdogo wa wadi ya Chwele.